Headlines News :
USWAZI MAGAZINE
Home » » HUYU NDO KIONGOZI ALIYEKUWA NA HESHIMA KULIKO VIONGOZI WOTE NCHINI NIGERIA AMBAE AMEFARIKI DUNIA.

HUYU NDO KIONGOZI ALIYEKUWA NA HESHIMA KULIKO VIONGOZI WOTE NCHINI NIGERIA AMBAE AMEFARIKI DUNIA.

Written By Unknown on Friday 6 June 2014 | Friday, June 06, 2014


Kiongozi wa waisilamu katika jimbo la Kano nchini Ngeria,Al-Haji Ado Bayero, amefariki.
Kiongozi huyo mwenye kuheshimiwa sana miongoni mwa viongozi wengine wote nchini humo , amethibitishwa kufariki nchini humo.
Al-Haji Ado Bayero, alikuwa mtawala wa Kano tangu mwaka 1963 na alifariki baada ya kuugua kwa mda mrefu.
Tangu wakati huo Nigeria imekabiliana na misukosuko ya mapinduzi ya kijeshi na ghasia zingine.
Alikuwa na umri wa miaka 84 na kutambuliwa kama kiongozi wa muda mrefu sana na mkongwe zaidi wa waisilamu katika jimbo hilo na pia alitambulika kama kiongozi wa pili mwenye ushaiwishi zaidi kwa waisilamu Nigeria
Marehemu Emir pia alitambuliwa kama kiongozi aliyependa amani.
Miaka miwili iliyopita alinusurika kwa tundu la sindano baada ya msafara wake kushambuliwa ambapo dereva wake na walinzi wake wawili walifariki.
Ilishukiwa kuwa kundi la wapiganaji wa kiisilamu wenye itikadi kali, Boko Haram, ndio waliomshambulia.
Boko Haram wamewashutumu viongozi wa kijadi nchini Nigeria kwa kuwa vibaraka wa wanasiasa. Juma lililopita Emir wa Gwoza aliuliwa na kundi hilo ambalo limetekeleza mashambulizi mengi Kaskazini Mashariki mwa nnchi hiyo.
Mwandishi wa BBC Sa'ad Abdullahi mjini Abuja anasema kuwa emiralikuwa amerejea tu kutoka mjini London ambako alikuwa anapokea matibabu.
Maishani mwake alikuwa mfanyakazi wa banki, polisi, mbunge , balozi na mfanyabiashara maarufu.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
Share Na Jamaa Yako :

0 comments:

Toa Maoni yako

Tuambie Unafikilia Nini..!

Followers

Facebook Fan Page

Tukutane Twitter

Walio Tembelea Website Hii

Advertise

Smiley face
 
Support : Ismail Niyonkuru | Gody Godwin Unstoppable
Proudly powered by Blogger
Copyright © 2011. Ahabona 24 - Haki Zote Zimehifadhiwa
Template Design by Gody Godwin Unstoppable Published by Uswazi